Friday, July 2, 2010

Them, I & Them......UNITED STATES OF AFRICA.....Innocent Galinoma

The flag of the African Union. 54 stars for each country on the continent, it looks like a flag for the United States of Africa.
"If all Africa should unite, we'll be strong than any nation..... There will be no more WAR, there we'll be no more apartheid....."
Haya ni maneno aliyoanza nayo Innocent Galinoma katika wimbo wake mwanana UNITED STATES OF AMERICA ambao ndio zungumzo letu la leo kuhusisha fikra za msanii na maisha yetu ya sasa.
Mara nyingi katika kipengele hiki huwa naelezea mtazamo ama fikra ama uchambuzi wa nyimbo za wasanii wa Reggae nikihusisha na maisha ya sasa. Lakini wakati huu niliwaza na kuona ni vema nikampa nafasi msanii husika aeleze kwa undani kilichomsukuma kuandika wimbo huu wa UNITED STATES OF AFRICA ambao kila nikiusikiliza naona kama una suluhisho la matatizo mengi japo wenye kustahili kuyaona wanazidi kupuuza ili wanufaike. Kumbuka alivyosema Bob Marley kuwa "see they want to be the star, so they faight the tribal war". Kwa hiyo naamini watawala wanajua chenye uwezo wa kuleta amani, bali wanataka kunufaika na VITA.
Maswali yangu kwa Inno Galinoma ni kuwa
CHANGAMOTO YETU: "Katika Albamu yako KILIMANJARO umeimba nyimbo zenye maswali mengi kwa Afrika na waAfrika (mfano Africans, Kilimanjaro na hata Running). Na katika albamu hiyohiyo umetoa baadhi ya suluhisho ambazo zingeweza kuwa msaada mwema kwa bara letu na waAfrika kwa ujumla kama katika wimbo huu United States of Africa.
Unapoangalia maisha yalivyo sasa ikiwa ni zaidi ya miaka 18 tangu utoe wimbo huo na matatizo uliyoyazungumzia yakingalipo na suluhu ulizoshauri hazionekani kufuatwa japo twajua zingekuwa msaada ama mwisho wa matatizo, UNAJISIKIAJE na hii inaweza kuathiri vipi kuendelea na fani hii?"
Na bila hiyana, Inno alikuwa mwepesi na wa haraka tena mwenye ukarimu kunijibu maswali yangu haya na hii ni sehemu ya majibu yake.
INNOCENT GALINOMA: "nilipotunga na kuimba United States Of Africa ilikuwa ni kama ndoto tu ambayo nilikuwa nayo, na nilidhani labda baada ya ukoloni kwisha na nchi zote za Afrika kuwa huru, ingekua ni rahisi na bora kuungana na kuliita taifa letu moja, kubwa ambalo litajumuisha nchi zote za Afrka. United States Of Afrika ingewezekana kama wote tungekuwa na mawazo sawasawa, lakini unaelewa kuwa hiyo ni ndoto, hata ndugu wa Baba mmoja mara nyingine hawaelewani. Mfano, wakati wa enzi za Mwalimu (Julius Nyerere), (Jommo) Kenyatta, na (Milton) Obote, ilikuwa ni kama mwanzo mzuri, umoja wa East Afrika ungeendelea kukua kwa kuongeza nchi moja moja ambazo zilikuwa na fikra sawa, kwa mfano Zambia, uhusiano wetu nao ulikuwa ni mwema, pamoja na Msumbiji, pamoja na nchi ambazo Tanzania ilijitoa kwa hali na mali na pia damu kwa ajili ya ukombozi wa hizi nchi. Lakini matokeo yake tunayaona leo, nchi nyingine zinajigawa, mfano Eritrea na Ethiopia. Somalia hata serikali inayoeleweka haipo, na hata kwetu Tanzania, nyumbani, Zanzibr wakati mwingine inaonekana kama inataka kujitenga na bara kwa sababu zisizoeleweka. Suluhu haitapatikana iwapo matabaka ya watu yananza kujitokeza nchini, kuna wale walio nacho, na wanacho kwelikweli, na wale wasio nacho wanakanyagwa na wenye nacho. Miaka imeenda sana na Afrika imebadilika kwa mema na kwa mabaya. Ukoloni bado upo na wakati huu mkandamizaji sio mzungu tena, bali ni WaAfirika we nzetu.
La mwisho, najisikia vibaya sana kuona jinsi baadhi ya wananchi hali yao ya maisha ilivo, I mean, People suffer so much just to live little life or just to survive in Africa, and That is a shame beacause Africa is rich. Unapoangalia mbele utaona wazi ya kuwa Africa inanunuliwa kimpangompango bila ya wanachi kujua kinachoendelea, japo mara moja moja utasikia kiongozi fulani amebakwa yuko mahakamani na magazeti na TV zikitangaza..... Almasi, Dhahabu, Tanzanite zitakuwa zinondolewa Afrika kwenda kwenye masoko ya nje bila ya wananchi kufaidika na chochote.
Nina Dada, shangazi, na mashemeji kibao, lakini sija wahi kumwona hata mmoja wao, amejiremba na Tanzanite."
KUHUSU HAYA YOTE KUATHIRI KAZI ZAKE AMA ZA AINA YAKE:
"ni kweli hii imeathiri sana utunzi na uimbaji wa nyimbo za aina yangu, la kwanza, ni kawaida kwa wasikilizaji hasa wenye umri mdogo na ambao ndio wengi, kutosikiliza nyimbo ambazo zinabeba ujumbe unaogusia maisha au matatizo,au kero za kisiasa ama magonjwa kama ukimwi na kadhalika. Wengi wanataka kusikia nyimbo zinazoburudisha na kuchekesha, kama wote tulivokuwa vijana. Wanataka kusikia na kucheza nyimbo ambazo zinazungumzia mabinti wa jirani, au bling bling, ama migari mikubwa mikubwa ama nyumba kubwa na "usafiri" wa mabinti na zaidi.... iko haja ya kuwahusisha vijana wajao, wenye vipaji na mawazo au fikra za kuburudisha na kuelimisha na kutangaza amani upendo na majambo yanajo husu jamii na mazingira na Tanzania na Africa kwa ujumla."
Sina ninaloweza kuongeza hapa. Blogu ya Changamoto yetu yamshukuru saana Kaka Inno kwa kutushirikisha kilichomsukuma kutunga, kinachoendelea kuumiza moyo wake kutokana na kutotatuliwa kwa matatizo na kile aonacho chaja siku zijazo.
Usikilize wimbo huu kiukamilifu hapa chini.

**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

4 comments:

José Ramón said...

Hongera kwenye ukurasa wako na makala Nawapongeza ninyi!Inayohusiana na ...
Abstraction maandiko na kutafakari

Anonymous said...

Job well done Mr Bandio...Innocent is one among few musicians wanaothubutu kuongea sense na ukweli kwenye nyimbo zao..bila kujali.Congrats kwa kupata hii exclusive.

Mike Mhagama/LA.

Fadhy Mtanga said...

Kaka,
Kila nitembeleapo blog yako huwa napata mambo mengi sana. Nakushukuru kwa hii United States of Africa. Ama kwa hakika ni wimbo wenye akili sana.

Nakutakia Jumapili njema wewe na familia yako.

Yasinta Ngonyani said...

Kibaraza hiki kina Changamoto Ahsante kwa wimbo United States of Africa. Kila la kheri.